UHABA WA WALIMU MJUMUISHO NI CHANGAMOTO KUBWA KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU MASKULINI

Wazara  elimu na mafunzo ya amali Zanzibar imetakiwa kuwafundisha walimu wengi elimu mjumuisho  ili wawe na uwezo wa kuwasomesha wanafunzi wenye ulemavu maskulini.

Hayo yamesemwa na mama wa Mtoto mwenye ulemavu wa viungo Siwawi Omar Said wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko nyumbani kwake  Kijichame wilaya ya Micheweni Pemba, amesema walimu wengi wanaofundisha maskulini hawana taaluma ya kufundishia wanafunzi wenye ulemavu.

Amesema watoto wenye ulemavu wamekuwa wakipata shida, kwani hawaelewi wanachofundishwa, hivyo ni vyema wizara ya elimu kuwafundisha walimu lugha mbali mbali kulingana na mahitaji ya mlemavu mwenyewe.

‘’Ni vyema kuwepo na walimu wenye taluma ya kufndisha walemavu, kwani bila kufanyiwa hivyo wanakua hawaelewi lolote watakua wanakwenda wakicheza tu huko maskulini,’’ Alisema mama.

Wadau wa elimu mjumuisho kisiwani Pemba wameiomba Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar kupitia taasisi ya elimu kuangalia uwezekano wa kuingiza somo la watu wenye ulemavu kwenye mtaala wa elimu visiwani hapa ili kutoa  hamasa  ya kufanya vizuri kwa wanafunzi wenye  ulemavu.

‘’Nivyema  somo la watu wenye ulemavu likaingizwa kwenye mtaala wa elimu, kwani kutawafanya walemavu waweze kufahamu vizuri masomo yao wanapo fundishwa’’,  wameeleza Wadau.

Kwa upande wake Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar  wa Kisiwani Pemba  Ahmed Abuubakar  amesema  mtaala uliopo  sasa ni  changamoto  kubwa  kwa  elimu mjumuisho.

Nae Afisa elimu mjumuisho pemba Ali Khamis Kombo amekiri kuepo kwa changamoto ya upungufu wa walimu wa elimu mjumuisho maskulini.

Hivyo amewataka wazazi kuwa na subra kwani wizara iko kwenye mchakato wa kuhakikisha elimu mjumuisho imeingizwa kwenye mtaala ili kuona walimu wote wanapotoka vyuoni wana utaalama ya kufundisha wanafunzi wenye ulemavu.



 

                                                                                               

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.