TASISI ZA KIHABARI ZATAKIWA KUWEKA SERA ZA UDHALILISHAJI

 

NA FATMA HAMAD FAKI.

Mwenyekiti wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania [TAMWA] Joic  Shebe  amesema kuweko na mfumo maalum ambao utawasaidia wandishi wa habari kuripoti malalamiko yao wakati wanapofanyiwa unyanyasaji wa kingono katika tasisi zao.

Mwenye kiti huyo ameyasemahayo katika mdahalo kuhusu unyanyasaji wa kingono katika tathnia ya habar  kwa wandishi wa habari uliofanyika kwa njia ya mtandao amesema bado wandishi wa habari wanawake wanakumbana na unyanyasaji wa kingono wakati wanapokua katika harakati zao za kazi.

Amesema kwa mujibu wa utafiti uliofanywa unaonesha kuwa kila  penye watu wawili mmoja amefanyiwa unyanyasaji, hivyi ni vyema kwa vyombo vya habari  vitunge sera  na kuhakikisha zinafuatwa kwa mujibu wa sheria ili kutoa adhabu kali kwa wale watakao jihusisha na vitendo hivyo.

Akiwasilisha mada ya sera ya jinsia katika vyombo vya habari  Nevil Meena  amesema wandishi wa habari ndio mwanga kwa jamii, hivyo wasikubali kufanyiwa unyanyasaji wa ngono kwa ajili tu ya kujipatia maslah.

Mapema Afisa  program wa Baraza la habari Tanzania [ MCT] Zanzibar Shifaa Said Hassan amesema kwa mujibu wa utafiti ulioufanywa umeonyesha kuwa vyombo vingi vya habari havina sera ya unyanyasaji, hivyo ipo haja kuwepo na ufuatiliaji wa hali ya juu ili kupata tarifa sahihi za unyanyasaji kwa wandishi wa habar.

Naibu waziri wa habari Tanzania  Paulina Gekul amesema kila mzazi anatamani mtoto wake atimize ndoto zake bila vikwazo vyovyote ,hivyo basi ni budi kila mmoja kwa nafasi yake alionayo awe mlinzi na mlezi kwa mtoto wa menzake.

Aidha amewasihi wandishi wa habari wanawake wajiheshimu, kujilinda na kufuata maadili yao kwani kufanya hivyo kutawaepusha na udhalilishaji.

Nae  priska  Ishamba mwandishi na mtangazaji wa wa Cloud tv amewashauri wandishi wenzake wasivunjike moyo wakati watakapo pata  vikwazo kama hivyo bali watoe tarifa na waendelee kuchapa kazi ili hali tu wafuate sheria na madili yao.

Mdahalo huo kuhusu udhalilishaji katika tasisi za habari kwa wandishi wa habari umeandaliwa na Jukwa la wahariri Tanzania kwa kushirikiana na shirika la Internws Tanzania.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.