.AJIRA BADO NI KIKWAZO KWA WATU WENYE ULEMAVU
NA FATMA
HAMAD PEMBA.
JAMII ya
watu wenye ulemavu kisiwani Pemba wanalalamikia upatikanaji mdogo wa furusa ya
ushirikishwaji katika mambo mbali mbali ya kimaendeleo katika jamii ikiwemo suala
la ajira.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Chake chake mwenyekiti wa jumuia ya watu wasiona ZANAP Suleiman Mansour amesema watu wa jamii hiyo wamekua
wakiwekwa nyuma katika fursa za kimaendeleo wakati
zinapotokezea katika jamii au za kiserikali ikiwemo suala zima la nafasi za ajira.
‘’ ushiriki
wa watu wenye ulemavu katika sekta ya Ajira bado ni wa kusuwa suwa sana,
Alidai mwenyekiti”.
Amesema ni
vyema kwa Serikali kuweka mpango mkakati wa kuhakikisha kuna kuwepo na idadi
stahiki ya watu wenye ulemavu katika nafasi mbali mbali za uajiri.
Mratibu wa idara ya watu wenye ulemavu Pemba
Mashavu Juma Mabrouk amesema sheria ya watu wenye ulemavu imesema walemavu
wanahaki sawa ya kupata ajira, hivyo
idara yake imekua ikifanya kila jitihada ili kuona watu wenye ulemavu na
wao wanapata fursa sawa wakati zinapotokezea.
Hivyo amewataka watu wenye ulemavu wasikate tamaa
kutokana na hali walizo nazo bali wajiendeleze kielimu jambo amblo litawasaidia
kukidhi vigezo vinavo stahiki katika mfumo mzima wa ajira.
Comments
Post a Comment