SIGARA NA TUMBAKU HUSABABISHA MARADHI YA SARATANI YA SINGO YAKIZAZI, KENSA YA DAMU NA KISUKARI KWA WATUMIAJI WA VILEO HIVYO
Amesema
imebainika kuwa wengi watumiaji wa Sigara na Tumbaku hupata maradhi ya Kisukari, Kensa,Ugonjwa wa akili
na ugonjwa wa moyo.
‘’Tumbaku ni
hatari jamani ukiitumia kwa kuvuta ama kwa kutafuna’’ alisema Bi Zuhura.
Amesema kuwa
shirika la Afya ulimwenguni limesema zaidi ya watu milioni 8 hufariki dunia
kila mwaka ulimwenguni kutokana na matumizi ya tumbaku ambapo kati hao milioni 7 wanaofariki ni wale wanaovuta ama
wanaotafuna.
Ameleza kuwa
zaid ya watu Bilioni moja nukta tatu ya wathirika wa tumbaku ni kutoka katika
Nchi zenye kipato cha chini.
‘’Sisi Nchi
zetu ndio zaid watu wanathirika na matumizi ya tumbaku’’ alisema Bi Zuhura.
Kwa mujibu
wa utafiti uliofanywa Zanzibaer mwaka
2011 umeonyesha kwamba kila penye watu 100 watu 7 wamebainika kuwa wanajishuhulisha
na matumizi ya Sigara ambapo wengi wao ni wanaume.
Akifungua
mkutano huo Afisa mdahini wizara ya Afya, Ustawiwa jamii Wazee Jinsia na Watoto Yakoub Mohd Shoka amesema Serikali
ya mapinduzi ya Zanzibar imeanzisha Sheria na kanuni ya udhibiti wa matumizi ya
tumbaku, Sigara katika maeneo ya wazi ikiwemo kwenye Dala dala, Sokoni na
katika sehemu za starehe ili kupunguza madhara yanayotokana vileo hivyo.
Aidha
amesema ni marufuku kwa mtu yoyote kuuza, kusambaza kutengeneza, kuonesha tumbaku
bila ya kuingiza katika vifungashio maalum ambavyo vinaonesha tumbaku ni hatari
kwa afya yako.
Samba mba na
hilo amesema kwa mujibu wa sheria na kanuni ni marufuku kwa mtoto chini ya
miaka 18 kujishuhulisha na uzaji au ununuzi wa bidha ya tumbaku.
Comments
Post a Comment