WADAU WA KUPINGA UDHALILISHAJI WAWAPIGA MSASA WANAOSULUHISHA KESI ZA UDHALILISHAJI MAJUMBANI KWAO.
NA FATMA HAMAD PEMBA 12/4/2021.
Jamii
imetakiwa kuondosha muhali na kuachatabia ya kufanya suluhu majumbani kesi za udhalilishaji jambo ambalo linapelekea kuongezeka kwa
matendo hayo.
Akitoa elimu kwa wanafunzi na wazazi huko
skuli ya Muambe wilaya ya mkoani juu ya
athari za utdalilishaji msaidizi wa
sheria shehia ya mkanyageni Haji Shoka
amewataka wanafunzi pamoja na
wazazi kuzipeleka katika vyombo vya sheria kesi za udhalilishaji.
Amese licha
ya elimu inayotolewa kwa jamii juu ya madhara ya udhalilishaji
lakini bado kunabaadhi ya wazazi wanazifanyia suluhu majumbani kesi hizo kwa kuhofia ugomvi katika familia zao
hali ambayo inawakosesha haki zao
wahanga wa matendo hayo.
‘’Wazazi
acheni ubishi kimbilieni kwenye vyombo vya sheria wakati unapotokea
udhalilishaji’’ Alisema msaidizi wa sheria.
Amesema wakati umefika kwa Wazazi na Walezi
kushirikiana na vyombo vya sheria juu ya kesi hizi za udhalilishaji ili
kuondosha unyama huu ambao wanaendelea kufanyiwa Watoto siku hadi siku.
Aidha amewanasihi
wanafunzi wa skuli ya Muambe kutoa
tarifa kwa Walimu na wazazi wao pindi wanapoona udhalilishaji
unafanyika katika skuli zao bila ya woga
wowote kwani kufanya hivyo kutasaidia kuondosha matendo hayo kijijini kwao.
‘’Wanafunzi
musimuogope mtu hatakama ni mwalimu, ni mjomba wako ukiona ana vitendo vibaya
toa tarifa achukuliwe hatua’’ Alisema Haji Shoka.
Ameeleza
Elimu ndio msingi wa maisha hivyo ni budi kuachana na tabia hatarishi na badala
yake kushuhulikie masomo yao ili kupatikana Taifa lenye wataalamu katika Sekta
mbali mbali ikiwemo Afya na Elimu.
Comments
Post a Comment