TAMWA INAENDELEA KUWAPIKA WANAJAMII JUU YA UTHUBUTU WA KUSIMAMA MAHAKAMANI KUTOA USHAHIDI.


 NA FATMAN HAMAD PEMBA.

Jamii imetakiwa  kusimama  kidete mahakamani kutoa ushahidi katika kesi za udhalilishaji ili  kuhakikisha watuhumiwa wa makosa hayo wametiwa hatiani na kupata adhabu.

Akizungumza na wananchi wa Chokocho wilaya ya Mkoani Pemba katika mkutano wa uhamasishaji juu ya umuhimu wa kutoa ushahidi Ali Amour Makame kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka [ DPP]  Chake chake amesema kesi nyingi zinakwama mahakamani kutokana na kukosa ushahidi.

Amesema  wengi wafanyaji wa matukio hao ni watu wa karibu na familia, hivyo wengi wanashindwa kwenda mahakamani kwa kuhofia ugomvi katika familia zao.

‘’Jamii  hawataki kutoa ushahidi wanaogopa watu wao  kufungwa  kwani wengi wanaofanya udhalilishaji ni watu wa karibu Ami, Baba wa kambo,  Mjomba na kadalika.

Amesema Bila ya kupatikana ushahidi unaostahiki hakuwezi kuwa na kesi hivyo  ni  vyema jamii kuacha muhali  na waweko tayari kushirikiana na vyombo vya sheria ili kuwafichua wahalifu wanaowahujumu watoto na kuondokana na tatizo hilo.

Mapema Afisa Dawati la Jinsia kutoka  wilaya ya Mkoani Rehema  Mjawiei amesema kama jamii haitoacha muhali juu ya kesi hizi kutapelekea kuongezeka  kwa udhalilishaji na kupatikana kwa watoto mabaradhuli.

‘’Hali ni tete jamani ya udhalilishaji, acheni muhali ili tuweze kuwanusuru watoto wetu,’’ Alisema Afisa dawati.

Hivyo amewataka Wazazi na walezi kushirikiana kwa pamoja katika malezi na kufuatilia nyendo za watoto wao ili kuwalinda na udhalilishaji.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo  wamewataka wahusika wa vyombo vya sheria wanaoshuhulikia kesi hizo kuziendesha kwa uwadilifu wa hali ya juu na kutoa adhabu kubwa kwa watendaji wa makosa hayo kwani kutasaidia kuondokana  na matendo hayo.

Mratibu wa chama cha wandishi wa habari Wanawake Tanzania Zanzibar [Tamwa]  ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Saidasema lengo la mkutano huo ni kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa  kuripoti na kutoa ushahidi mahakamani pindi itakapotokezea udhalilishaji katika maeneo  yao wanaoishi.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.