TALAKA ZACHANGIA UDHALILISHAJI KWA WATOTO
Akizungumza
na Pemba ya leo Katibu wa kamati ya Madili kupitia baraza la Tasisi za Kislamu
Zanzibar Abdala Mnubi Abasi amesema imebainika kuwa wanandoa wengi wanapoachana
mzigo mkubwa wa malezi humuangukia mama peke yake hali ambayo kunakosekana kwa huduma
bora kwa Watoto.
Amesema kukosekana
kwa malezi ya pamoja ya Baba na Mama watoto hukosa matunzo stahiki na kuamua kujiajiri wenyewe
hali ambayo inasababisha kufanyiwa udhalilishaji.
‘’Inapovunjika
ndoa Watoto husambaratika kwani mababa
hawatoi tena huduma’’, Alisema katibu wa madili.
Amesema
imebainika kuwa wengi wafanywaji wa matukio hayo ni watoto ambao wamekosa
malezi ya pamoja kutokana na wazazi wao kuachana.
Katibu huo
amewataka wanajamii kuwa na subra wakati inapotokezea migogoro ya kifamilia na
kutafuta suluhu mbadala ili kuepusha talaka za ovyo ovyo jambo ambalo
litawafanya watoto kuishi maisha ya
amani na kuepukana na udhalilishaji.
Comments
Post a Comment