SERIKALI YATAKIWA KUCHUKUA HATUA KALI ZA KISHERIA KWA WALE WOTE WANAOZIFANYIA SULUHU KESI UDHALILISHAJI


NA FATMA HAMAD PEMBA

Serikali ya mapinduzi zanzibar imetakiwa kuwachukulia hatua kali za  kisheria  wale wote watakaobainika wanazifanyia suluhu majumbani kwao kesi za udhalilishaji kwa watoto.

Hayo yamesemwa na wanafunzi wa skuli ya chokocho wilaya ya mkoani pemba katika mkutano wa kushajisha jamii juu ya umuhimu wa   kutoa  ushahidi mahakamani kwa kesi za udhalilishaji.

Wamesema  bado wapo  wanafamilia  wanashindwa kwenda mahakamani kutoa ushahidi  na kuzifanyia suluhu wenyewe kwa wnyewe jambo ambalo linapelekea kuongezeka kwa udhalilishaji hapa nchini.

‘’tunaiomba serikali kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaoharibu ushahidi kwa makusudi.

Kwa upande  wake  mwanafunzi  isha hassan ibrahim kutoka skuli ya sekondari  chokocho  amesema wakati umefika kwa wazazi na walezi kuwa mstari mbele kuzisimamia ipasavyo kesi hizo ili kuona wabakaji wanatiwa hatiani.



Akitoa elimu kwa wanafunzi hao juu ya athari za utdalilishaji  msaidizi wa sheria  shehia ya mkanyageni shaban  ali  amewataka wanafunzi  kujiepusha na vikundi viovu ambavyo vinasababisha kufanyiwa udhalilishaji.

Aidha  amewataka wanafunzi hao kushuhulikia masomo yao ili waweze kupata ufalu mzuri katika mitihani yao.







 

 

 



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.