MABARAZA YA YATAKIWA KUCHAGUA VIONGOZI WAPYA WENYE SIFA
Wajumbe wa mabaraza ya Vijana Zanzibar wametakiwa kuchagua viongozi imara ambao wataendesha vyema mabaraza hayo.
Akizungumza
na wajumbe wa mabaraza ya vijana kisiwani Pemba Afisa mdhamini Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Salum Ubwa Nassor katika mkutano wa
tathimini wa baraza hilo tangu lilipoanzishwa mwaka 2016 hadi 2021 huko Gombani
Chake chake Pemba.
Amesema bila
ya viongozi wenye sifa hawawezi kulifanya baraza kufikia katika maendeleo
yaliokusudiwa katika kuanzishwa kwake.
‘’Niwaombe
wajumbe mliopo kwenye baraza na mliostafu kutafuta wenye viti na makamo wapya
ambao wataliendeleza baraza hilo’’ amesema mdhamin ubwa.
Akifafanua
kua viongozi wa mabaraza yaliopita walifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani
waliweza kuongeza vijana wengi katika mabaraza yao.
Amesema
lengo la tathmini hiyo ni kuona wajumbe wapya watakaochagulia kuendesha
mabaraza ya vijana yajao kuwa wazalendo na wadilifu katika utekelezaji wa
majukumu yao ambayo yanaendana na Serikali ya awamu ya Nane.
Comments
Post a Comment