BINTI WA MIAKA 15 AMBAE NI MWANAFUNZI WA DARASA LA TANO APEWA UJAUZITO KWA MARA YA PILI NA SHEMEJI YAKE PEMBA.
Mtoto wa miaka 15 apewa ujauzito kwa mara ya pili huko Wilaya ya Mkoani Mkoa
wa Kusini Pemba
Waswahili
husema mchovya asali hachovi mara moja. Ni hakika hii ndio kawaida kwani asali
ladha yake ni tamu na kama utaendekeza kuchovya basi huenda ukamaliza kibuyu.
Mimi kwa
hapa naulinganisha msemo huu na wale wanopenda kupata mazuri kwa njia ya mkato
bila kujali athari zinazoweza kujitokeza, kwani akifanya mara ya kwanza
akifanikiwa bila kupata tatizo lolote basi kwake hujenga mazowea na akaendeleza
tabia yake bila kujali kwamba atajiharibia au kumuharibia anaemfanyia uovu
hule.
Na haya ndo
aloyafanya kijana Mosi Othman Mosi mkaazi wa Muambe Wilaya ya Mkoani huko
Kisiwani Pemba.
Kijana huyu
bila huruma wala kujali athari za anaemfanyia amediriki kwa mara mbili
mfululizo kumpa ujauzito mtoto wa miaka 15 mbaye kwa sasa yupo darasa la tano.
Alianza kumfanyia
unyama huu akiwa darasa la nne ambapo kwa wakati huo alikuwa ana umri wa miaka
kama 13 hivi na msichana huyu mdogo alilazimika kukatisha masomo ili alee
ujauzito wake hadi pale alipojifungua.
Kwa Rehma za
Alla alijifungua salama usalmin bila shida yoyote na akafanikiwa kupata mtoto
wa kiume. Baada ya kujifungua kamati ya elimu katika eneo lake ilimnasihi mtoto
huyu ili arudi skuli kujiunga na wenzake aendelee na masomo nayeye akakubali
kufanya hivyo.
Masikini
mtoto wa watu aliendelea na masomo kwa matumaini lakini kumbe yule adui wa
maisha yake kwa vile yupo na anamuona akanza tena kutumia ulaghai wa maneno na
kumuahidi vitu tofauti ikiwemo kufunga nae ndoa hivyo nae bila kujijuwa akanasa
katika mtego kwa mara nyengine tena.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi huko nyumbani kwao huku akiwa anabubujika machozi
na kulia kwa kwikwi mtoto huyo amesema
yote haya yalijitokeza kwa vile hadi familia yake ilikuwa hampi msaada hata wa
kumlea mtoto wake wakati yeye anapo kwenda skuli hali ambayo ilimfanya akatishe
masomo miezi sita tuu baada ya kurudi skuli alipokwisha kujifungua.
Mtoto huyo
mwenye muonekano mdogo wa umbo na umri huku akiwa analea mtoto mwenziwe ambaye
hajuwi hata namna ya kumuhudumia wote wawili wanaonekana kuchoka kwa idhilali
ya maisha.
Na kwa upande wa kiafya wote wawili kimtazamo
wa macho afya zao haziko vizuri kwani hicho kichanga kinaonekana kudhofu sana
na ngozi yake kujaa vidonda vinavyo ashiria kukosa matunzo stahiki kwa mtoto
mchanga.
Pamoja na
muonekano huo kinachosikitisha zaidi ni kuwa kisichana hicho chenye umri wa
miaka 15 pamoja na idhilali hiyo tayari anujauzito usiopungua miezi mitano huku
mtenda makosa hayo akiwa hajulikani alipo.
Kwa
masikitiko ali mueleza mwandishi wa habari hizi kuwa kabla ya kumpa ujauzito wa mara hii ambayo ni ya pili alimuambia ananmpenda
amkubalie anayoyataka kwani atafunga nae ndowa.
‘’Aliniahidi
atanioa ila mwisho wa siku ameshakimbia hajanio’’ Alieleza mtoto huyo.
Aidha
amesema anaishi katika mazingira magumu hawezi kumudu kujihudumia yeye mwenyewe
pamoja na mtoto wake.
Amesema amekuwa akipata mateso pamoja na manyanyaso
kutoka kwa familya yake kutokana na masahibu hayo ambayo yamemkuta
Hivyo amevitaka vyombo vya sheria kuchukua hatua kali kwa mtuhumiwa huyo ambae amekatisha ndoto za maisha yake.
Mapema mama mzazi wa mtoto huyo aliebakwa na kupewa ujauzito amesema kesi hii ya pili ipo kituo cha polisi Kengeja ingawa kwa kesi ya kwanza ilifika mahakamani lakini haikupata ufumbuzi wowote kwani ilidaiwa kuwa haina ushahidi.
Hivyo
amelitaka Jeshi la Polisi kumsaidia kumtafuta mtuhumiwa huyo ili aweze
kuchukuliwa hatua za kisheria.
‘’Serikali
imtafute mtuhumiwa mpaka apatikane’’ Alisema mama mtoto.
Nae baba
mzazi wa mtoto huyo amesema yuko tayari kushirikiana na vyombo vya sheria ili
kuona mtuhumiwa huyo ametiwa hatiani na mtoto wake kupata haki stahiki.
Sheha wa shehiya hiyo Fatma Khamis Ali amesema nikweli mtoto huyo wa miaka 15 ambae ni mwanafunzi wa darasa la 5 ana ujauzito wa miezi 5 ambapo ujauzito huo ni wa mara ya pili, na inasemekana alompa ujauzito huo ni yule yule alompa mara ya kwanza na ni mtu wake wa karibu.
‘’saa hizi
angekuwa darasa la sita nae kama wenziwe ila yeye ndo kanfikwa ni mitiani kama
hiyo.’’alisema sheha huyo.
‘’Tukio la
kwanza ambapo ekuwa darasa la nne nililipeleka kituo cha Polisi Kengeja na kesi ikafika mahakamani lakini haikupatiwa
ufumbuzi kwa sababu eti ilikosa ushahidi, na mchovya asali hachovi mara moja
tunkaa kashafanya tena vile vile’’alisema sheha huyo huku akieleza kwamba kesi ya pili nayo ipo hapo hapo kengeja ambapo wamesema mtuhumiwa anatafutwa.
Sheha huyo
aliendelea kumueleza mwandishi wa habari hizi kwamba hili ni tukio la pili la
wanafunzi kupewa ujauzito ikiwa mmoja ni mwanafunzi wa darasa la kumi na moja,
kupewa ujauzito kuanzia januari hadi April mwaka huu katika shehia yake.
Kufuatia
malalamiko ya kwamba kesi hizi za udhalilishaji kwa baadhi ya shehia imekuwa
ngumu kupatiwa hukumu tulimtafuta Kamanda wa Polisi mkoa wa Kusini Pemba Ahmed
Khamis Makarani ambapo amesema endapo mtu amefungua kesi yake katika kituo cha
Polisi na akiona hapewi mrejesho wowote asibakie
nyumbani bali afuate taratibu hadi kufikia makao makuu mpaka ahakishe
kesi yake imepatiwa ufumbuzi.
Mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar [ Tamwa] Ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said amesema wamekua wakitoa Elimu kwa wanajamii kuhakikisha kesi za aina hii wanazisimamia na kuzitolea ushahidi ili watuhumiwa waweze kutiwa hatiani kitu ambacho kitasaidia kuondoa tatizo la udhalilishaji kwa jamii.
‘’Naiomba
jamii wasikubali kusuluhisha kesi za udhalilishaji katika Serikali za Shehia nahata katika Vituo Vidogo
vya Polisi kwani huwa hakuna hukumu na ndio mana ukaona watuhumiwa kila siku
warudia makosa hayo hayo’’ alisema Bi Fathiya.
Msaidizi
Afisa ustawi wa wanawake na Watoto kutoka wilaya ya Mkoani Aisha Abdi amesema bado kesi hiyo
haijaripotiwa katika ofisi yake na kuwataka waathirika wa tukio hilo kufuata
taratibu za kuiripoti ili wasaidiane katiaka kutafuta haki ya muathirika.
Matukio ya udhalilishaji katika shehia ya Mwambe na Kengeja yanaonekana kushamiri kwani katika kipindi cha mwaka jana pia kuna mwanafunzi wa darasa la sita alipewa ujauzito na mtu wake wa karibu kama ilivyo kwa yule wa darasa la tano ambaye mtuhumiwa hajulikani alipo.
Jumla ya kesi 174 za udhalilishaji zimeripotiwa katika Vituo mbali mbali vya Polisi Mkoa wa Kusini Pemba kuanzia Januari hadi Disemba mwakajana kati ya hizo 88 ziko kwenye upelelezi, 27 zimefungwa, 44 ziko mahakamani, na moja imeondolewa, ambapo za Watoto wanaokinzana na sheria 11 zipo upelelezi, 2 zimefungwa na moja inaendelea mahakamani, Na kuanzia January hadi March mwaka huu ni jumla ya 55 zimefunguliwa katika vituo hivyo vya Polisi.
Comments
Post a Comment