Umaskini ni moja ya chanzo za udhalilishaji.
UMASKINI uliokithiri imebainika kuwa ni moja ya
sababu inayopelekea Watoto kufanyiwa
Udhalilishaji.
Hayo yamesemwa na mdau wa mtandao wa
kupinga udhalilishaji kutoka Wilaya ya Mkoani, katika mkutano wa uwasilishaji
wa ripoti za utekelezaji wa majukumu yao ya kutoa elimu juu ya madhara ya udhalilishaji wa kijinsia
kwa jamii uliofanyika ofisi ya TAMWA Pemba.
Kwa upande wake Shaaban Juma Kassim Msaidizi
wa sheria kutoka shehia ya Mkanyageni,
alifahamisha kuwa udhalilishaji unafanyika
zaidi kwa watoto wanaokosa malezi
ya pamoja ambao wazazi wao wameachana.
Alisema
takribani watoto wengi ambao wazazi wao wameachana, wanakosa
masomo na badala yake wanatumikishwa ili wapate mahitaji yao hali ambayo inarudisha nyuma maendeleo ya watoto.
‘’Wanawake wengi hususan wanaoishi vijijini
ni maskini, hivyo hushindwa kuwalea watoto ipasavyo na kupelekea kudhalilishwa’’,alisema
Shaaban.
Nae Afisa Tathmini na ufuatiliaji wa chama
cha Wandishi wa habari Wanawake
Zanzibar Mohamed Khatib Mohamed,
amewataka wadau hao waendelee
kuzifuatilia kesi, ambazo wameziibua
wakati walipokuwa wakitoa elimu.
Comments
Post a Comment