Kamati ya Madili ya Baraza la Habari Tanzania-MCT-imesema ni marufuku kwa mujibu wa sheria ,Mandishi wa habari kuvaa sare za cha siasa .

 

Kamati ya Madili ya Baraza la Habari Tanzania-MCT-imesema ni marufuku kwa mujibu wa sheria ,Mandishi wa habari kuvaa sare za chama cha siasa  wakati anapotekeleza majukumu yake hasa katika kipindi hichi cha kampeni za uchaguzi.

 Hayo yamesemwa na Katibu mtendaji wa baraza la habari Tanzania Kajub Mkajanga katika Mkutano wa Wandishi wa Habari na Vyanzo vya habari uliofanyika  katika ukumbi wa mikutano wa kiwanja wa michezo GombanChake chake Mkoa wa Kusini Pemba.

Amesema sio jambo zuri kwa Mwandishi  wa habari kuvaa sare za chama kwani inaweza kuhatarisha usalama wake na vyombo vyake pamoja na kituo anachokifanyia kazi.

‘’Kwa mujibu wa sheria ya tume ya uchaguzi ni kosa kisheria mwandishi kuvaa sare ya chama, hili pia hata sisi MCT tunapiga marufuku hivyo hakikisheni mnajiepusha na vitewndo hivyo”alisisitiza.

Aidha amesema mtu yoyote atakae mlazimisha  mwandishi  kuvaa nguo ya chama atakuwa amevunja Sheria  na kanuni za uandishi wa habari.

Amefahamisha kuwa  wandishi endapo  watavaa nguo za chama wakati wa napokua katika shuhuli zao za kihabari watambue kwamba wanahatarisha maisha yao.

Mapema makamo mwenyekiti wa kamati ya maadili kutoka baraza la Habari Tanzania [MCT]  Eda Sanga amewataka wandishi wa habari kuandika habari zao kwa kufuata Kanuni na Misingi ya kihabari.

Wakitaja  changa moto ambazozinawakabili  baadhi ya wandishi walioshiriki  mkutano huo wamesema ni kukosa mashirikiano mazuri kwa baadhi ya Tasisi  wakati wanapokwenda kupata habari

Samba mba na hayo wamelitaka Baraza la Habari  MCT kuwapa taaluma Viongozi wa Tasisi mbali mbali zikiwemo za Serikali na Binafsi ili kufahamu umuhimu na mchango wa Wandishi wa habari.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.