MAADHIMISHO YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI ZANZIBA KUFANYIKA MEI 17
Na Fatma Hamad- Pemba Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) imesema Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani yanategemewa kufanyika Jumamosi tarehe 17 Mei, 2025 katika ukumbi wa RAHALEO STUDIO kuanzia saa 2:30 asubuhi ambapo yatahudhuriwa na waandishi wa habari, wadau mbali mbali wa habari pamoja na wawakilishi kutoka taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali. Makamo mwenyekiti wa kamati hiyo Dkt. Mzuri Issa amesema kuwa maadhimisho ya mwaka huu yana ujumbe muhimu na adhimu ambao ni “Sheria nzuri ya Habari ni chachu ya uchaguzi ulio huru na wa haki” Maadhimisho hayo ni muhimu katika kukuza na kuimarisha kada ya habari hapa nchini pamoja na kutoa wito maalum kwa...