Posts

Showing posts from November, 2025

“Uchumi, unavyofifiza Ndoto za Wanawake Wenye Ulemavu kufikia uongoz’’

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA Katika kipindi cha uchaguzi wa mwaka 2025, Tanzania imeshuhudia wimbi jipya la wanawake wenye ulemavu wanaojitokeza kugombea nafasi za uongozi  kutoka udiwani, ubunge hadi uwakilishi wa majimbo. Ingawa  nyuma ya safari hiyo ya kisiasa, kuna simulizi  ya kiuchumi, unavyosababisha  wanawake hao kufikia malengo yao ya kisiasa. Makala hii inachambua jinsi uchumi wa wanawake wenye ulemavu unavyoathiri ushiriki wao katika maamuzi, nafasi zao za uongozi, na sauti yao katika jamii ya Tanzania, hususan Zanzibar, kwa kuzingatia takwimu, sheria, na mikataba ya kimataifa. Utafiti wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wa mwaka 2022, unaonesha zaidi ya asilimia 73 ya watu wenye ulemavu nchini, wanafanya kazi katika sekta zisizo rasmi hususan kilimo, uvuvi na biashara ndogondogo.  Maranyingi, wanawake wenye ulemavu wanabaki nyuma zaidi kwa sababu ya changamoto hiyo ya uchimi, mitajina ukosefu wa fursa za kifedha, hali hii huwafanya kushindwa kughar...

MRADI WA SWIL ULIVYOLETA MABADILIKO KWA WANAWAKE WENYE ULEMAVU PEMBA

Image
  NA FAMA HAMAD, PEMBA Mradi wa kuwawezesha wanawake kudai haki zao za uongozi , demokrasia na siasa (SWIL)  umeandika historia mpya katika visiwa vya Zanzibar, umeleta nuru na matumaini kwa wanawake, hususan wale wenye ulemavu, waliokuwa kwa muda mrefu wakihisi kusahaulika katika safari ya maendeleo na uongozi. Mradi huo ulizinduliwa rasmi mwaka 2020 na unatarajiwa kumalizika Disemba 2026 umeonekana na mafaniko makubwa katika hatuwa mbalimbali za utekelezaji wake.   Utekelezaji huo wa (SWIL) ni ushirikiano kati ya  TAMWA-Zanzibar ,  ZAFELA ,  JUWAUZA , na PEGAO , umewafikia wanawake zaidi ya  4,000  katika wilaya za Pemba na Unguja, ukiwajengea uwezo, ujasiri, ari na ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi. Lengo kuu la mradi ni kuongeza ushiriki wa wanawake, ikiwa ni pamoja na wanawake wenye ulemavu, katika michakato ya uongozi, siasa na demokrasia Zanzibar (Unguja na Pemba) hivyo kuwawezesha kuwa “watendaji hai” badala ya kuwa ka...