Wanafunzi wapewa mbinu ya kujikinga na udhalilishaji
NA SALIM HAMAD, PEMBA Wanafunzi wametakiwa kutoa tarifa kwa watu wao wa karibu wakati wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji ili kuweza kujulikana na kuchukuliwa hatua. Hayo yamesemwa na Msaidizi wa Sheria shehia ya Tumbe mashariki wakati akizungumza na wanafunzi wa Skuli ya Shumba vyamboni katika mkutano malummu ulioandaliwa na Jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Micheweni Pemba. Alisema vitendo vya udhalilishaji hufanyika kila sehemu ikiwemo Madrasa, Skuli,Majumbani,hivyo ni budi kutoa tarifa wakati watakapofanyiwa. ‘’Msiyafiche matendo ya udhalilishaji hata kama mmefanyiwa na watu wenu wa karibu akiwemo mwalimu,kaka Mjomba toeni tarifa msione aibu’’,alisema. Mapema msaidizi wa sheria shehia ya Tumbe Mashariki Fatma Hamad Faki aliwasisitiza wanafunzi hao wasipoke zawadi ya aina yoyote wanazopewa na wat...