WIZARA YA AFYA WATOA USHAURI KWA WANDISHI WA HABARI

 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wandishi wa habari wamehimizwa  kuendelea  kuielimisha  jamii  kufahamu  umuhimu  wa  chanjo  ili waweze kujitokeza  kwa wingi vituo vya afya  kupata  chanjo jambo ambalo litawaepusha na  maradhi mbali mbali  ikiwemo shurua,  Saratani ya shingo ya kizazi  pamoja  na  Korona.

Wito huo umetolewa na Afisa mdhamini wizara ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali katika mkutano wa tathmini ya huduma wa mpango  wa chanjo zinazotolewa  Zanziba  ya  mwaka  2022  kwa  wandishi  wa  habari  huko  baraza  la  mji  Chake  chake  Pemba.

Amesema jukumu kubwa la wandishi wa habari ni kuielimisha jamii katika masuala mbali mbali ya kimaendeleo, hivyo ni wakati  kwa wandishi wa habari kuwafahamisha wananchi kupata chanjo zinazotolewa na wizara ya Afya kwa usahihi ili kuepusha vifo vya watoto na jamii kiujumla.

‘’Ndugu zangu wandishi wa habari tunawaomba mtusaidie kuifahamisha jamii wawapeleke watoto wao wapate chanjo ili kuwakinga na magonjwa hatarishi’’ alieleza afisa mdhamini.

Aidha amefahamisha kuwa licha ya kiwango cha chanjo kuwepo juu lakini bado kuna tatizo  la mabinti wengi walio katika umri wa miaka 14  hawapati  chanjo  ambazo  zitawakinga  na maradhi tofauti ikiwemo saratani ya shingo ya kizazi kutokana na uwelewa mdogo uliopo katika jamii kwa.

Mapema mkuu wa kitengo  cha chanjo ofisi ya Pemba Bakar Hamad amesema kuwa chanjo zote zinazotolewa na wizara ya afya ziko salama hazina madhara yoyote, hivyo wazazi wawachomeshe watoto wao bila ya woga wowote.

Amesema kwa mwaka  huu wa  2023 wizara imejipanga kutoa huduma ya chanjo hadi maskulini ili kuhakikisha watoto wote na wasichana wamepatiwa chanjo hizo.

Nae mkuu wa kitengo cha huduma za Chanjo Zanzibar Abdul hamid Ameir Saleh amewataka wandishi wa habari kushirikiana na kitengo cha chanjo  na kurusha habari  zinazo husu kitengo hicho ili  wananchi  waweze kuchukua hatua  ya kujikinga dhidi ya maradhi hatarishi.

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.