wandishi wa habari watakiwa kuepuka kuandika habari zinazo wadhalilisha watu wenye ulemavu

 

NA FATMA HAMAD PEMBA 9/3/ 2022.

Wandishiwa habari wametakiwa kufuata miko na madili ya kazi yao wakati wanapoandika  na kuripoti habari za watu wenye ulemavu ili kulinda utu, heshima ya kundi la watu hao.

Akizungumza  katika mkutano wa kuwajengea uwezo wa kuripoti habari za watu wenye ulemavu  wandishi wa habari wa Unguja na Pemba huko hoteli ya Maru maru Juma Salum Ali kutoka   Shujuwaza amesema watu wenye ulemavu wanahaki ya kulindwa, kuheshimiwa na kuthaminiwa kama  watu wengine.

‘’Niwaombe  sana  epukeni kutumia majina mabaya wakati mnapoandika na kuripoti habari za watu wenye ulemavu  ambayo yanaleta viashiria vya udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu’’ alisema Juma Salum.

Kwa upande wake Ussi Khamis  ameeleza kuwa watu wenye ulemavu bado wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma za kijamii ikiwemo Ajira Elimu na kushika nafasi za uongozi, hivyo  ni vyema wanahabari kupaza sauti zenu  kuzisemea kero hizo hali ambayo itasaidia kuondosha matatizo hayo.

Nao wandishi wa habari walionufaika na mafunzo hayo wamesema kundi kubwa la watu wenye ulemavu wenyewe bado hawazifahamu sheria  wala haki zao stahiki  ambazo wanatakiwa na wao wazipate , hivyo ni budi kwa jumuia zinazoshuhulikia watu hao kuwapa elimu ili waweze kufuatilia wakati wanaponyimwa haki zao.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.