wandishi wa habari wahimizwa kuandika habari za watu wenye ulemavu

 


NA FATMA HAMAD PEMBA      8/3/ 2022.

Wandishi  wa  habari  wametakiwa  kujikita zaid maeneo ya  Vijijini ili kuibua kero na changamoto ambazo zimekuwa zikiwakumba watu wenye ulemavu.

Wito huo umetolewa na Waziri wanchi ofisi ya makamo wa kwanza wa rais Zanzibar Saada Mkuya Salim wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa wandishi wa  habari wa  vyombo mbali mbali  Zanzibar  huko ukumbe wa Maru maru Hoteli kisiwani unguja.

Alisema  watu wenyeulemavu wamekuwa wakikumbana na matatizo mbali mbali hivyo ni wakati wandishi kujitoa na kuzibua  kero ili ziweze kufikia kwa jamii na kupatiwa ufumbuzi.

‘’Nyinyi wandishi wa habari  mnamchango mkubwa wa kubadilisha maisha ya watu wenye ulemavu hivyo msikae tu bali nendeni mkaibuwe  na muweze kuyatoa katika vyombo vya habari jambo ambalo litamfanya kila aneguswa na hilo aweze kutimiza majukumu yake kwa mujibu wa nafasi yake alionayo’’ alieleza waziri.

Kwa upande mwengine waziri sada aliwasihi wazazi ambao wana watoto wenye ulemavu kuacha tabia ya kuwafungia ndani watoto hao kwani nawao wanahaki ya kupata mahitaji mbali mbali ikiwemo Elimu na Uongozi kama watoto wengine.



Mapema  mkuu wa program kutoka shirika la Internews Tanzania Shaban Maganga alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo na kuwapatia mbinu mbadala  ambazo zitawawezesha  kuandika na kuripoti habari za watu wenye ulemavu jambo ambalo litaleta  mabadiliko kwa watu hao.

Nae   Mkuu wa mradi mjumuishi  wa Vyombo vya Habari kanda ya Afrika Jackie  lidubwi  amewataka waandishi wa Habari kuwashirikisha watu wenye ulemavu kwa kuwapa nafasi za kueleza shida zao wakati wanapoandika habari zao.



Aidha aliwashauri wandishi wa habari kutumia majina sahihi wakati wanapoandika na kuripoti habari za watu wenye ulemavu ambayo hayataleta athari kwa watu hao katika jamii.

Baadhi ya wandishi walioshiriki mkutano huo wamewataka watendaji wa Internews kuendelea kutoa  mafunzo mbali mbali ikiwemo ya lugha za alama jambo ambalo  litawazesha  wandishi hao  kuzungumza na kuibua kero za watu wenye ulemavu wa aina zote.

Mafunzo hayo ya siku mbili yaliyoshirikisha waandishi kutoka Unguja na Pemba yamelenga kuongeza uwelewa kwa waandishi wa Habari katika kuripoti habari zinazohusu watu wenye ulemavu Visiwani Zanzibar.




 

 

 

 

 

 

 

 


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.