WAZAZI WAHIMIZWA KUWAPATIA ELIMU WATOTO WENYE ULEMAVU


 Wazazi na walezi wenye watoto walemavu wametakiwa kuwapeleka mashuleni pamoja  na madras ili waweze kupata elimu ambayo itawafaa katika maisha yao ya badae.

Ushauri huo umetolewa na mmoja wa mzazi wa mtoto wenye ulemavu wa viungo  hapa kisiwani Pemba amesema watoto wenye ulemavu nawao wana haki ya kupata elimu kama watoto wengine.

Amesema wapo wazazi wamekua wakiwafungia ndani, watoto wao wenye ulemavu, jambo ambalo limekua likiwakosesha fursa mbali mbali ikiwemo elimu.

‘’Nawaomba wazazi wenzangu msiwafungie ndani watoto walemavu, kwani mkiwaeka ndani watakua wanadumaa na mnawatia maradhi, Alisema mama mwenye mtoto mlemavu.

Amefihamisha kuwa watoto walemavu maranyingi hufanya  vizuri katika masomo yao ukilinganisha na wengine wasio na ulemavu.

Akitoa ushuhuda amesema wakati mtoto wake  mlemavu hajapata kigari cha kuendea shule alikua hachangamki na alikua akiwaona wenzake wanakwenda shule akijitia chumbani na kulia.

Hivyo kwa sasa amefanikiwa kupata kigari, anakwenda shule na anachangamka na wenzake,  tofauti na pale alipokua haendi shule.

Kwa upabnde wake Afisa  wa elimu mjumuisho  Ali Khamis  Kombo amesema wizara imeanzisha elimu mjumuisho katika shule za mjini na Vijijini ili kuona watoto wenye ulemavu na wao wanapata haki yao ya elimu.

Nae mratibu wa idara ya watu wenye ulemavu ofisi ya Pemba Mashavu Juman Mabrouk  amesema wameweka mikakati madhubuti  wa kutoa elimu kwa jamii ili kuona watoto waenye ulemavu wanapata haki zao za msingi ikiwemo Elimu, Afya.



 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.