AFUNGWA KWA KUBAKA


 

 Kushindwa kudhibiti matamanio yake kumempelekea  Kijana Thani Khamis Mohd 22 mkaazi wa Kinyasini Mkoani Pemba kutumikia Chuo cha Mafunzo kwa muda wa miaka 14, pamoja na fidia ya shiling milioni mbili  (2,000,000)/.

Hakimu wa mahakama ya mkoa A Chake chake Abdul Razak Abdul kadir amesema hukumu hiyo imekuja baada ya mahakama yake kujiridhisha kutokana na ushahidi uliotolewa na mashahidi.

Hivyo mahakama imeamua kumtia hatiani mtuhumiwa huyo, na endapo atashindwa kulipa fidia atatumikia tena kifungo cha miezi 6.

‘’Mahakama yangu imeridhika na ushahidi uliotolewa ndipo ikatoa hukumu na endapo atashindwa kulipa fidiya atatumikia tena kifungo cha miezi 6,’’ alisema hakimu.

Mwendesha  mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka Seif Mohamed Khamis amekubaliana na hukumu hiyo, kwani itakua ni fundisho kwa wabakaji.

Aidha amewataka wananchi kushirikiana na mahakama kutoa ushahidi  ili kuona kesi za udhalilishaji zinapata hatia jambo ambalo litapunguza vitendo hivyo katika Jamii.

Awali iIielezwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa huyo  siku ya terehe 21 /7/ 2018 majira ya saa 7:00 mchana huko eneo la Mkirikiti Kinyasini wilaya ya Mkoani, Pemba  alijaribu kutaka kumbaka msichana wa miaka 12.

Kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha 111[1] [2], [a] cha sheria nambari 6 ya 2018, sheria ya Zanzibar.



 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.