WANANCHI WAHIMIZWA KUWAPELEKA WATOTO VITUO VYA AFYA KUPATA CHANJO


Wizara ya Afya Zanzibar imewataka Wananchi kujitokeza kwa wingi kuwapeleka watoto wao katika Vituo vya Afya ili kupata chanjo jambo ambalo litawakinga Watoto na maradhi mbali mbali ya mambukizi ikiwemo Pepopunda na Kifaduro.

Akizungumza na Wandishi wa habari huko ukumbi wa Maabara Chake chake Pemba Afisa Mdhamini wizara ya Afya Ustawi wa Jamii Wazee Jinsia na Watoto Yakoub Mohd Shoka amesema zoezi la utoaji wa chanjo litanza rasmi tarehe 26 hadi 30 mwezi huu katika Vituo vyote vya Afya vilivyomo wilaya zote Visiwani hapa.

Amesema  kila mwisho wa  mwezi wa Nne ya kila mwaka, ni wiki ya chanjo ya Afrika ambapo kwa Zanzibar  wizara ya Afya huadhimisha  zoezi la utoaji wa chanjo za kawaida kwa Watoto na akinamama ili kua na jamii isio na mambukizi ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ‘’Chanjo huweka Jamii pamoja’’.

Amesema lengo la Chanjo hizo ni kuhakikisha Watoto wote wanapatiwa, ili waweze kuondokana na maradhi hatarishi ikiwemo Saratani ya mlango wa kizazi, Polio, kifua kikuu, Surua, na kifaduro.

Amefahamisha kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imedhamiria kufanya jitihada mbali mbali za makusudi ili kuona Watoto wote wanaishi wakiwa na Afya nzuri.




Kwa upande wake mratibu wa huduma ya  chanjo za Mama na Mtoto Pemba Bakar Hamad Bakar amesema licha ya juhudi mbali mbali zinazochukuliwa na Serikali ili kuona Watoto wanaondokana na maradhi ya mambukizi lakini bado wanajamii wanamuhali juu ya chanjo hizo kwa.

Hivyo amewahimiza Watoto wote wenye umri wa miaka 14 kufika vituoni kupatiwa chanjo  ili kujikinga na mambukizi ya  maradhi ya Saratani ya mlango wa kizazi.



 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.