KOCHA wa timu ya Waawi Star Kasim Ali Kasim amesema atautumia mfungo wa ramadhani kwa kukifua kikosi chake ili kiwefiti katika michano ya ligi daraja la kwanza kanda ya Pemba,itayoendelea tena mara baada ya mfungo wa Mwezimtukufu wa ramadhani.

 

KOCHA wa timu ya Waawi Star Kasim Ali Kasim amesema atautumia mfungo wa ramadhani kwa kukifua kikosi chake ili kiwefiti  katika michano ya ligi daraja la kwanza kanda ya Pemba,itayoendelea tena mara baada ya mfungo wa Mwezimtukufu wa ramadhani.

Wawi Star ambayo ilishawahi kushiriki  ligi kuu ya Zanzibar, msimu wa mwaka juzi iliyaanza mashindano hayo kwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Mkoroshoni United katika  mchezo uliopigwa uwanja wa Gombani Kisiwani hapa.

Akizungumza na Mwanaspoti Kocha huyo alisema licha kuwa Vijana wake wapo kwenye swaumu lakini atakitumia kipindi cha mapunziko ya ligi kwa kufanya mazoezi ya kufa mtu kuona wanafanya vizuri kwenye mzunguko wa pili.

Alisema katika mzunguko uliopita aliona udhaifu mkubwa kwenye  kikosi chake hasa katika sehemu ya umaliziaji kiasi cha kumfanya kocha huyo kuamua  kuutumia mwezi huu wa mfungo kukiandaa kikosi chake.
‘’Kkipindi hichi cha ramadhani hatutolala tutahamasishana kufanya mazoezi kuona yale mapungufu yaliyojitokeza katika mzunguko wa kwanza yanaondoka tuweze kufanya vizuri kufanya vizuri katika mzunguko ujao’’alisema.

Katika hatua nyengine Kocha huyo aliwasifu waamuzi waliochezesha mzunguko wa kwanza kwa kuchezesha vizuri kwa kila timu kupambana kiuwezo wake .

 ‘’Ligi imenza vizuri waamuzi walichezesha mzunguko wa kwanza watayafanya mashindano hayo kuwa na ubora na yenye ushindani mkubwa na  kuepusha uvunjifu wa amani viwanjani uliokuwa unajitokeza vizuri hakuna timu iliyokuwa inalalamika saana kuwa imeoneowa tunawaomba waamuzi wajitahidi kuzifuata sheria za Soka  ili kulinda heshma zao  na kuepusha na lawama  viwanjani’’alisema.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.