MASHEHA WATAKIWA KUWACHUKULIA HATUA WANAOVURUGA AMANI NCHINI
NA FATMA HAMAD, PEMBA Mwenyekiti wa kamati ya madili Zanzibar Abdala Mnubi Abasi amewataka Masheha kushirikiana na kamati hiyo kuondosha vitendo viovu vinavyofanywa na watu wasio kuwa na khofu ya Mungu katika jamii zao, ili kulinda amani na silka za kizanzibar. Mwenye kiti huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na Masheha wa wilaya ya Wete huko ofisi ya mkuu wa Wilaya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba. Alisema katika Ramadhani ya mwakajana waligundua jumla ya vituo 14 ambavo vilikua vinapikwa mchana wa mwezi mtukufu wa ramadhani kisiwani Pemba. ‘’Hata kama mtu si muislamu lakini hatakiwi kupika na kula mchana hadharani, hivyo niwaombe Masheha kuchukuwa hatua watu ambao wanakula kinyume na taratibu zilizowekwa na Serikali,alisema. Aidha alisema katika mji wa Wete kuna vibanda ambavyo vinatumiwa na Mama ntilie kwa ajili ya kuuzia biashara zao, lakini ikifika nyakati za usiku vibanda hivyo hutumika kama ni sehemu za starehe, hivyo aliwataka masheha kuweka ulinzi shirikishi kati